UPAMBAJI WA ENEO LA KULA CHAKULA ( DINING AREA)

blogger templates
Leo tuingie upande wa dining area, katika chumba hiki wengi wetu katika nyumba hua kinaangaliana na sitting room, na kwa wachache hua wamekitenga yaani kinakua na ukuta hukioni.....

Tuanze na kwa hawa ambao dining inaonekana......katika ukipamba chumba hiki, angalia kwanza unahitaji kiweje yaani kiwe na mandhali gani, na kisha angalia ni nini na nini ni cha kuondoa. kama kimechakaa ama kimekwisha, ondoa ili uweze kupata nafasi nzuri kwa kuweza kudesign.

Kwa wale wenye dining room inayojitegemea unaweza paka rangi tofauti maana humu kunajitegemea......

Ingia mitandaoni, ama nunua magazines za home deco...angalia mipangilio iliyoko huko na mpaka rangi.....halafu ukisha jua ni nini unataka, viandike, na uanze kutafuta, sasa hapa waweza kuja kwa mtaalamu wa mambo ya decorations (Homez Deco) ama ukafanya mwenyewe.

Fanya window shopping kwanza, na uangalie pia na ukubwa wa dining area yako.....wengi wetu tuna eneo dogo lakini bila kujua ama wengine hawajali, wanaweka meza kubwa ya watu 6 wakati eneo ni lakuweka meza ya watu 4.....hili jamani tuwe makini katika hili....(Kufanya window shopping inakusaidia kufanya manunuzi ndani ya budget uliyopangilia)

Contemporary Dining Room by Denver Architects & Designers Ashley Campbell Interior Design






Tukishajua na kupata mpangilio mzuri.....sasa paka rangi yako, na hakikisha rangi iwe kwenye kundi ama isipishane sana na ile ya sitting room yetu, hii ni kwa dining area ambayo inaangaliana na sitting room...

Hakikisha pia kama unapaka rangi ambayo ina kiza basi paka ukuta mmoja na taa ziwe ni za kutosha, na pazia zisiwe na giza, hakikisha pia madirisha yako yanaingiza mwanga wa kutosha,  na kuta zingine ziwe zina rangi ambayo ina mwanga maana isije kuleta giza hata mchana.........kwa upande wa fanicha pia waweza kuchanganya zikawa na rangi mbili...maana tumezoe tuu kufananisha seti ya viti inakua ni moja tuuu kwa upande wa rangi......waweza kuweka carpet pia iendane.........ingawa sio lazima kuweka carpet.....
Contemporary Dining Room by Fort Lauderdale Architects & Designers tuthill architecture


Mara nyingi hua tunapendelea sisi wataalamu wa decoration, kuweka chandalier dining area, maana inaleta mvuto wa aina yake katika chumba hiki, na isishuke sana, kuna vipimo vya kuweka ili hata mtu mrefu akinyanyuka asijigonge.......Mara nyingi Dining hua hatutakiwi kuweka furniture nyingi ili kuonekane kumependeza.......kabati lako, ama console table na kioo chake ama picha kwa juu kama hutaki kioo,  meza yako ya chakula, carpet ukipenda, maua juu ya meza, taa ya chandalier, pazia zako. Naomba tuangalie mifano hii ya dining katika picha na uone kama kumejazana furnitures humu, na ndipo mtakapo kubaliana nami kua hata vitu vichache hupendeza pia......

0 Response to "UPAMBAJI WA ENEO LA KULA CHAKULA ( DINING AREA)"

Posting Komentar