Dawa Ya Mende....

blogger templates
hongera sana kwa kazi nzuri unayofanya. nina shida moja nahitaji msaada wako nyumbani kwangu kuna mende sana kila sehemu , kama unaweza kujua dawa nisaidie hili nilitatue hili tatizo.  nijibu kupitia blog yako.

asante sana
mimi-Anna 


Homez Deco tumepata email hii kutoka kwa mdau wangu na anaomba usahuri kama inavyosomeka.....Na napenda kumjibu hivi.....

Unachotakiwa kufanya ni kutafuta sababu ya mende kuwa katika nyumba yako, na sababu ni kati ya hizi, :
1. hauweki vitu kwa mpangilio
2. nguo ni nyingi na ziko katika malundo
3. hautumii products nzuri za usafi
4. uchafu uliokithiri
5. mabaki ya chakula hayatupwi sehemu husika na kwa usafi
6. usafi pia haufanyiki ipasavyo etc...
Hizi ni baadhi ya points ambazo ningependa uzifanyie kazi.....kuanzia nje mpaka ndani....na inahitajika uache kazi ufanye kazi, nikiwa nina maana kua ujitolee siku moja ufanye usafi wa nyumba nzima.......ikiwezekana utoe vitu nje vipigwe na jua kwa muda hata wa siku mbili ama tatu, na ndani ufanye fammigation pamoja na nje.....
Kabla ya kuingiza vitu ndani, hakikisha unachagua vitu unavyovihitaji, usivyo hitaji kama viko katika hali nzuri gawa, kama havifai basi tupa sehemu husika.......

This time ingiza ndani vitu utakavyotumia na upunguze mlundikano wa vitu.....na usafi uwe ni wa mara kwa mara, na kwasababu umefanya fammigation, ile ni sumu fanya usafi vizuri........

NB:
Hakikisha unahusisha na majirani katika fammigation maana ukifanya wewe mende watakimbilia kwa wenzio. dawa ikiisha nguvu mende wanarudi.......

Homez Deco tunakaribisha ushauri zaidi.....


0 Response to "Dawa Ya Mende...."

Posting Komentar